Rais
John Pombe Magufuli leo September 25, 2016 ameungana na waumini wa
kanisa la Anglikana la Mtakatifu Albano wakati wa Ibada ya Jumapili
katika kuadhimisha siku ya Bwana ya 19 katika Pentekoste.
Rais JPM
amezungumza na waumini wa kanisa hilo na kuwashukuru kwa kuungana na
madhehebu mengine katika kuliombea amani Taifa. JPM aliyeongozana na
mkewe Janeth Magufuli katika ibada hiyo amesema madhehebu yote yamekua
na kazi kubwa na muhimu katika taifa na kwamba watanzania wote bila
kujali dini zao, itikadi za kisiasa, makundi na kanda zao wana wajibu wa
kuungana na viongozi wa dini katika kuombea na kulinda amani.
>>>Ninawashukuru
kwasababu mnaendelea kuliombea taifa hili, ninawashukuru kwasababu kila
siku mmekuwa mkipiga magoti na kumtanguliza Mungu mbele, ninawashukuru
kwakuwa mnaendelea kuombea amani ya nchi yetu na upendo udumu ndani yetu
sote.
Makanisa yote, dini zote, madhehebu yote, vyama vyote upendo tukiujenga ndio tutaiendeleza vizuri tanzania yetu:- Rais JPM
Katika ibada hiyo Rais JPM alitoa shilingi milioni moja kwaajili ya kuchangia vikundi vya kwaya vya kanisa hilo.
Post a Comment