Sept 21, 2016 majina ya wasanii
watakaowania tuzo za MTV MAMA 2016 yalitajwa huku Naseeb Abdul aka
Diamond Platnumz na kundi la Navy Kenzo pamoja na Alikiba ndio wasanii
wa Tanzania waliotajwa kuwania tuzo kubwa za Africa za MTV Africa Music
Awards 2016.
Sasa millardayo.com & Ayo TV imewapata Navy Kenzo huku wakayaongea haya>>>Tunashukuru
sana tumepata taarifa za MTV MAMA 2016 tumechaguliwa kwenye Best Group
yaani tumefurahia sana ni kitu ambacho kimetutia nguvu sana
Kimeonesha
jinsi gani kazi yetu ambayo tuliyokuwa tukifanya kwa muda mrefu ndio
imeanza kuleta matunda hayo kwahiyo tunashukuru sana, tutatoa maelekezo
katika mitandao yetu ili mashabiki wetu na wengineo wajue jinsi ya
kutupigia kura’
Unaweza ukabonyeza play kuwasikiliza Navy Kenzo furaha yao baada ya kutajwa kuwania MTV MAMA 2016
Post a Comment