Usiku wa Septemba 24 2016 jiji la
London lilikuwa busy kwa upande wa mashabiki wa soka kwani mashabiki wa
timu kubwa za Arsenal na Chelsea walikuwa busy kufuatilia mchezo dhidi
ya vilabu vyao ambavyo vyote vinatokea ndani ya jiji la London.
Mchezo kati ya Arsenal dhidi ya Chelsea
ulichezwa katika dimba la Emirates, tofauti na ilivyozoeleka rekodi ya
Arsenal ya mechi 9 mfululizo kucheza dhidi ya Chelsea kushindwa kuibuka
na ushindi wowote na kuishia kutoa sare tatu na kati ya mechi hizo 9
alikuwa karuhusu kufungwa nyumbani mechi 2 na sare 3.
Hata hivyo rekodi za jumla zinaonesha
Arsenal amewahi kumfunga Chelsea mara 73 na kuwahi kufungwa mara 61,
wakiwa wamewahi kusuluhu mechi 54, mchezo wa Septemba 24 Arsenal
wameutumia kurudisha heshima yao na kuifunga Chelsea kwa goli 3-0,
magoli ambayo yalifungwa na Alexis Sanchez dakika ya 11, Theo Walcott dakika ya 14 na Mesut Ozil dakika ya 40.
Post a Comment