Septemba 24 2016 klabu ya Man United
ya England ilicheza mchezo wake wa sita wa Ligi Kuu England huku ikiwa
na kumbukumbu ya vipigo vitatu mfululizo, Man United safari hii ilishuka
katika dimba lake la Old Trafford kuikaribisha Leicester City ambao ni
Mabingwa watetezi wa EPL.
Tofauti na wengi walivyotegemea kuwa
huenda Man United wakapokea kipigo cha nne kutokana na kucheza na Bingwa
mtetezi Leicester City ambaye msimu uliopita aliwatoa jasho timu vigogo
wa EPL, leo wamefanikiwa kubuka na ushindi wa goli 4-1, kingine
kilichovutia ni mchezaji ghali zaidi duniani Paul Pogba alifunga goli
lake la kwanza.
Katika ushindi huo wa goli nne za Man United zilifungwa na Chris Smalling dakika ya 22, Juan Mata dakika ya 37, Marcus
Rashford dakika ya 40 na Paul Pogba ambaye alikuwa akibezwa kutokana na
kutofunga akafunga goli la nne dakika ya 42 na kuwaacha Leicester
wakiishia goli moja lililofungwa na Demarai Gray dakika ya 60.
Baada
ya ushindi huo wa Man United, kufunga goli kwa Pogba kulikuwa ni stori
katika mitandao ya kijamii, mshambuliaji wa KRC Genk Mbwana Samatta
alikuwa mmoja kati ya watu ambao walioneshwa kufurahishwa na kutumia
accout yake ya instagram kupost clip video iliyoambata na ujumbe wa
utani kuwa post hiyo imeletwa kwa hisani ya Pogba.
A video posted by Mbwana Samatta (@samagoal77) on Sep 24, 2016 at
Post a Comment