0
Uongozi wa klabu ya Liverpool upo kwenye mipango ya kumuongezea mkataba mwingine Mshambuliaji wake kutoka Misri, Mohamed Salah.

Taarifa zinaeleza kuwa Liverpool itakuwa inamlipa mchezaji huyo kasi cha paundi £200,000 kwa wiki na kuzima ndoto za Real Madrid kumpata nyota huyo.

Salah amesema anafurahia zaidi kuchezea soka lake katika Ligi ya England sababu inaendana na aina ya uchezaji wake.

"Naipenda EPL sababu inaendana na aina ya uchezaji wangu, napenda kucheza hapa" alisema.

Real Madrid inatajwa kuwa klabu iliyoweka nguvu nyingi za kumsajili nyota huyo ambaye anafanya vizuri kwenye msimu huu wa ligi akiwa na Liverpool.

Post a Comment

 
Top