September
22, 2016 mtu wangu wa nguvu, nakusogezea taarifa nyingine nzuri kutoka
kwa Davido star wa muziki kutoka nchini Nigeria ambaye alisaini deal na
ya kufanya kazi na lebo ya Sony Music. Taarifa hii nzuri ikufikie
shabiki wake uliyezimiss kazi za Davido kwenye Radio na TV.
Kimya
cha takribani miezi kumi na moja cha msanii Davido huenda kikamalizika
siku chache kutoka sasa, Hii ni baada ya star huyo anayesimamiwa kazi
zake na lebel ya RCA records iliyoko chini ya Sony Music, kupost video
akiwapa taarifa kuanza kuachiwa video zake zaidi ya 20 kabla mwaka 2016
haujaisha.
Davido
kupitia video hiyo amesema anapanga kwa kuumaliza mwaka 2016 kwa style
tofauti ili afanane na label yak, Sony Music ambao amedai kuwa
wamemruhusu kuanza kuachia kazi zake ikiwemo albam yake mpya itakayoitwa
Son of Mercy, ambayo itatoka ndani ya mwaka huu.
Davido alisaini
deal ya usimamizi wa kazi zake na kamouni ya Sony Music, January 20
2016 ambapo Taifa la Nigeria lilikua taifa la kwanza barani Afrika
kuingia makubaliano hayo na kuwa msanii wa kwanza wa Afrika kutia saini
ya record deal hiyo.
Post a Comment