0
Club ya Azam FC imefuzu hatua ya fainali ya michuano ya Mapinduzi Cup baada ya kuifunga Taifa Jang’ombe kwa goli 1-0 kwenye mchezo wa nusu fainali ya kwanza iliyochezwa kuanzia saa 10:15 jioni

Frank Domayo ndiye mfungaji wa bao pekee katika mchezo huo lililoivusha Azam na kuifanya icheze fainali na mshindi wa fainali ya pili kati ya Simba na Yanga itakayoanza saa 2:15 usiku kwenye uwanja wa Amaan, Zanzibar.

Mbali na kuifungia timu yake bao la ushindi, Domayo alitangazwa Man of the Match kutokana na kiwango chake kuwa bora katika mchezo huo.

Baada ya mchezo, Domayo alikabidhiwa kiatu cha kuchezea kama tuzo ya kuibuka mchezaji bora wa mechi lakini kama ilivyo utaratibu katika mashindano ya mwaka huu, alipatiwa crton nne za Malti kutoka kampuni ya Bakhresa.

Post a Comment

 
Top