Muigizaji wa filamu nchini, Shamsa Ford.
Muigizaji wa filamu nchini Shamsa Ford ametoa ushauri kwa
Watanzania hususani vijana ambao hupata kidogo na kushindwa kujipanga na
maisha ya kile kidogo wakipatacho na kusema siku zote unapaswa
kuthamini kile ulichonacho leo ili kuwa na kesho nzuri.
Shamsa Ford ametumia ukurasa wake wa Instagram kutoa ujumbe huo kwa
vijana na kuwaasa kutodharau kabisaa kidogo wakipatacho kwani hicho
ndicho kinaweza kufanya watu wapige hatua.
Wanapoteza muda wa sasa wakitarajia kuwa kesho ipo. Ukiona unadharau ‘kidogo’ ulichonacho kwa sababu ya kile ‘kikubwa’ unachotarajia, jua upo katika mchezo wa kufukuza upepo. Leo ni mbegu ya kesho unayoitarajia. Ulichonacho ndicho kimebeba mimba ya unachokitarajia. Usipokuwa mwaminifu kwa ulichonacho, sahau kuhusu unachotarajia" aliandika Shamsa Ford.
Post a Comment