0
Iran imetangaza kukubalia kikosi cha wanamieleka wa Marekani kushiriki mashindano ya dunia, yatakayofanyika nchini humo baadaye mwezi huu.

Awali Iran walisema kuwa wamarekani hawatakubaliwa kushiriki mashindano hayo.

Walinyimwa visa, baada ya Iran kusema kwamba itawapiga marufuku raia wa Marekani kama jibu kwa marufuku ya Rais Donald Trump kwa wairan kuzuru Marekani.

Wizara ya nchi za kigeni mjini Tehran, imesema kwamba, uamuzi wake wa sasa wa kuwakubalia wanamieleka wa Marekani ni sehemu ya uamuzi wa mahakama nchini Marekani kuahirisha kwa muda amri hiyo kuu ya Trump.

Post a Comment

 
Top