0

BARCELONA im­etajwa kuwa klabu ya soka inayoongoza kwa kuingiza fedha nyingi kuto­kana na malipo ya udhamini, ikiwa inaingiza pauni 187m kwa mwaka.

Barcelona inaingiza pauni 35m zaidi ya Manchester United na pauni 37m zaidi ya Real Madrid ambazo ndizo zinazofuatia ka­tika orodha hiyo.

Mapato yao mengi yaki­toka kwa Nike ambao wana mkataba nao wa pauni 88m kwa mwaka unaotara­jiwa kudumu hadi mwaka 2023.

Taarifa iliyotolewa na Jarida la Forbes imeelezwa Chelsea inashika nafasi ya nne ikiingiza pauni 102m, ikifuatiwa na Bay­ern Munich (pauni 91m), Paris Saint-Germain (pau­ni 76m).

Nyingine ni Arsenal (pauni 71m), Liverpool (pauni 70m), Tottenham (pauni 61m) na Manchester City (pauni 59m).

Post a Comment

 
Top