0
Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA kimelaani kitendo cha Jeshi la Polisi kumkamata Mwanasheria Mkuu wa Chama hicho na Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lisu kwa kile ilichodai bila kuzingatia kanuni na taratibu za Bunge huku ikilitaka Jeshi hilo kumwachia Mbunge huyo kwa dhamana.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaaam Katibu Mkuu wa CHADEMA Dk. Vicent Mashinji amedai kitendo kilichofanywa na Jeshi hilo cha kumkamata Tundu Lisu akiwa katika maeneo ya Bunge ni uvunjifu wa haki na Kinga za Wabunge ambapo amedai kuwa Jeshi hilo linatumika kuingilia siasa za Upinzani.
Wakati huhuo Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA kimezungumzia kuhusu Tuhuma zinazomkabili Mwenyekiti wa Chama hicho Freeman Mbowe kuhusiiana na kutajwa kwenye Orodha ya watu wanaotuhumiwa kuhusika na dawa za kulevya.

Post a Comment

 
Top