0
Mkoa wa Simiyu umetajwa kushika nafasi ya 64 katika uzalishaji wa zao la Pamba duniani ,ambapo hapa nchini unaongoza kwa kuzalisha kwa asilimia 50 ili kuweza kuwa Miongoni Mwa Mataifa 10 Bora ,Kilimo Kinapaswa kifumuliwe kiwe cha Kisasa pia Wakulima wahamasishwe kutilia mkazo kwenye pamba ya organiki ili kuongeza Mnyoyoro wa thamani wa zao hilo hasa katika Soko la dunia.
Akizungumza na Waandishi wa Habari Mara baada ya kuwasilisha Mwongozo wa uwekezaji Mkoani Simiyu katika kikao kilichowashirikisha wawekezaji wazawa ,wajumbe wa kamati za fedha na Uchumi wa Halmashauri sita ,Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi Watendaji lengo kuu ni uhamasishaji na kuendeleza uwekezaji ,Mtafiti Mwandamizi Taasisi ya Utafiti na Mambo ya Uchumi (ESRF) Bamwenda Gration ,
Amesema kuwa Simiyu ina fursa nyingi katika kilimo cha Mazao yenye thamani kubwa na yanayoweza kusindikwa ,kuchakatwa ,bidhaa zitokanazo na mifugo na maendeleo endelevu ya viwanda kuanzia viwanda vya bidhaa zitokanazo na Pamba Alizeti ,na Mazao ya Mikunde na ili kuongeza Pato la Mwananchi Simiyu ifikapo 2050 kutoka dola 3,600 hadi 12,000 lazima kilimo kiwe na tija .
Mkuu wa mkoa wa Simiyu Anthony Mtaka amesema mkoa unatekeleza miradi ambayo inalenga hasa katika sekta ya viwanda na tayari wilaya za maswa na meatu zimetoa nafasi ya umiliki wa mitazamo na umiliki wa dira kama mkoa na umiliki wa mawazo kwenda ngazi ya chini zaidi.

Post a Comment

 
Top