0
Kiteto.Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amewaagiza Mkuu wa Wilaya ya Kiteto, Tumaini Magesa na mkurugenzi wa halmsahuri ya wilaya hiyo, Tamim Kambona waende Kata ya Engusero Jumamosi wiki hii wakafanye mkutano wa hadhara na kujibu kero za wananchi wa kata hiyo.
Wametakiwa pia wafuatane na mwenyekiti wa halmashauri hiyo, Lairumbe Mollel wakatoe ufafanuzi bila kukosa.
Majaliwa ametoa agizo hilo leo katika kijiji cha Engusero wilayani kiteto baada ya kusimamishwa na wananchi wakati akiwa njiani kuelekea mjini Kibaya yalipo makao makuu ya wilaya hiyo ili aanze ziara ya kikazi ya Mkoa wa Manyara.
Akijibu baadhi ya maswali aliyoulizwa na wananchi wa kijiji cha Engusero, Waziri Mkuu amesema analichukua ombi la wakazi hao la kupata kujengewa

Post a Comment

 
Top