0

Chama cha Akiba na mikopo  cha  wananchi wa kijiji cha  Uswaa Mamba wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro ambao wanajishughulisha na kilimo na biashara ndogondogo kiko hatarini kufaa baada ya viongozi wa bodi kutuhumiwa kukopeshana akiba za wanancachama  zaidi ya shilingi milioni 100 kinyume cha sheria.
Wanachama hao wamesema  wanasikitishwa na hatua ya viongozi hao kusababisha ubathirifu huo ambao kwa sasa umesababisha wananchama hao kukosa mikopo ya kuwawezesha kufanya shughuli za maendeleo kama ilivyokusudiwa
Wamesema  kwa vema viongozi hao wakataifishwa mali zao kwa kuwa chama hicho kwa sasa kina mtaji wa shilingi milioni  25 ambazo hazitoshelezi kutokana na wengi wao kushindwa kupata mikopo  kwa ajili ya kulipia watoto wao ada,kilimo 
Afisa ushirika wilaya ya hai  bw. Paul ndulu amesema  viongozi hao watawajibishwa kutokana na  wao kuhusika  kusababisha hasara hiyo  ambayo imesababisha wananchama zaidi ya 1500 kukosa mikopo.
Meneja wa chama hicho bw. Shirilengwa ulomi  amethibitisha kuwepo kwa ubathirifu huo tangu mwaka 2013 ambapo viongozi walijiidhinishia fedha hizo kinyume cha sheria hali ambayo imesababisha chama hicho kuanza kuzorota.

Post a Comment

 
Top