0
VIPODOZI aina mbalimbali vyenye ujazo wa tani kumi, vimenaswa na kuzuiliwa katika kituo cha ukaguzi mizani ya Makambako mkoani Njombe vikielekea Jijini Dar es salaa.
Shehena hiyo imekutwa ikiwa katika magari mawili yote ya kampuni ya Kisima Company Limited. Ya jijini Dare s salaam iliyokuwa ikitokea nchini Kongo, katika tukio hilo watu watatu wanashikiliwa kati sita waliokuwemo ndani ya magari hayo wakiwemo madereva wawili na wasaidizi wao.
Magari hayo ni aina ya FAW yakusafirishia mafuta, yamekamatwa usiku wa februari 5 saa 5 za usiku yakitokea nchini Zambia kuelekea jijini Dar es salaamu.
Tukio hilo limehusisha gari aina ya FAW lenye namba T. 807 CHK na trela lenye namba T. 750 DDE na gari jingine namba T. 813 CHK yalikamatwa February 5 mwaka huu katika mizani ya Makambako.
Mhandisi Ruth Shallua ni msimamizi mkuu wa kituo cha mizani ametoa maelezo ya tukio hilo mbele ya mkuu wa mkoa wa Njombe, Cgrstopher Ole Sendeka na kamanda wa polisi Mkoa wa Njombe, Prodensia Protus ambao walifika kushuhudia tukio hilo katika kitupo cha polisi wilaya ya kipolisi Makambako.
Upande wake mkuu wa mkoa anasisitiza kupatikana kwa wathumiwa watatu waliotoroka mkono wa sheria.
Amesisitiza kujipanga kupambana na matukio kama hayo ikizingatia kuwa barabara hii huenda kuna magendo zaidi ya hayo yanafanyika pasipo kujulikana.
Uchunguzi zaidi wa mamlaka ya chakula na dawa umefika na kuendelea na ukaguzi wa mzigo huo, ili kutoa thathimini na thamani ya shehena hiyo.

Post a Comment

 
Top