0

WAKONG­WE wa soka nchini Italia, AC Milan wamefungiwa ku­shiriki michuano ya Ulaya kwa mwaka mmoja kuto­kana na kukiuka kanuni za soka.

Timu hiyo ilikuwa iki­jiandaa kushiriki katika mi­chuano ya Europa League msimu ujao wa 2018/19 baada ya kushika nafasi sita katika Serie A msimu uliopita.

Chanzo cha kufungiwa ni kukiuka kanuni ya masuala ya fedha (Financial Fair Play) am­bapo imeelezwa kuwa klabu hiyo imekuwa ikipoteza map­ato mengi kila mwaka kwa kutokuwa na hesabu nzuri za kifedha.

Milan inayonolewa na Gen­naro Gattuso ipo hatarini kupoteza mastaa wake wengi li­cha ya kuwa chini ya umiliki wa bilionea wa China, Li Yonghong. Shirikisho la Soka la Ulaya (Uefa) limetoa nafasi ya Milan kukata rufaa.

Post a Comment

 
Top